MAELFU ya wananchi wa Wilaya ya Arusha, wakiwemo wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamefurika katika ofisi za chama hicho kushuhudia na kumsindikiza mgombea wa ubunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Paul Makonda, wakati akichukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi hiyo kupitia CCM.
Baada ya kukamilisha zoezi hilo, Makonda aliwashukuru wananchi pamoja na makada wa chama kwa kumuunga mkono katika kila hatua, na kuahidi kuwa sauti na tumaini la wakazi wa jimbo hilo.




